• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

ZAIDI YA WANAFUNZI 29,000 WA SHULE ZA MSINGI WAPEWA DAWA ZA MINYOO

Posted on: April 18th, 2018


WANAFUNZI 29,000 wa shule za msingi katika Manispaa ya Moshi, wameanza kunufaika na mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele, baada ya Wizara ya Afya kuendesha zoezi maalumu la ugawaji wa dawa za minyoo ya tumbo na kichocho.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa hiyo, Michael Mwandezi aliyasema hayo jana, wakati akizindua rasmi zoezi hilo litakalozihusisha shule 35 za msingi.

Katika taarifa yake, Mkurugenzi huyo alisema walengwa wa zoezi hilo ni wanafunzi wenye umri kuanzia miaka mitano hadi 14.

"Tutatoa dawa hizo pia kwa watoto wa mitaani wanaoishi katika mazingira hatarishi ambao hawakuandikishwa," alisema Mwandezi.

Ugawaji wa dawa hizo katika shule za msingi umepangwa kufanyika Jumatano ya Aprili 10 na Alhamisi ya Aprili 19, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, magonjwa hayo ni sehemu tu ya magonjwa yale ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kama vile usubi, trakoma (ugonjwa wa vikope), matende na mabusha.

Hata hivyo, takwimu za Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa wanaoathirika zaidi ni wananchi wanaoishi katika mazingira ya umasikini, wanaozungukwa na mazingira machafu na wanaokutana na wadudu wanaosambaza vimelea vya magonjwa hayo.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba magonjwa hayo hayapewi kipaumbele kama magonjwa mengine ya Ukimwi (AIDS) na Kifua Kikuu (TB).

Mwandezi alisisitiza kuwa matatizo ambayo husababishwa na magonjwa ambayo hayapewi kipaumbele ni pamoja na utapia mlo, upungufu wa damu na upofu.

Mengine ni kuathiri ukuaji wa mtoto, gharama kubwa za matibabu, huathiri mahudhurio ya watoto shuleni na husababisha utumbo kuziba kwa minyoo.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi