• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

WANAWAKE NA VIJANA WAKOPESHWA MILIONI 334

Posted on: June 7th, 2018

Halmashauri ya manispaa ya Moshi, imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 334, kwa vikundi 47 vya wanawake,vijana na walemavu, katika manispaa kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/2018.

Hayo yameelezwa na mkuu wa Idara Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii  Rose Minja, wakati wa hafla ya kukabidhi hundi kwa ajili ya mikopo hiyo kwa vikundi 20 vya wanawake na vijana kwa robo yanne ya mwaka wa fedha 2017/2018.

Katika hafla hiyo iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Halamshauri, Minja alisema asilimia 72 ya mikopo iliyochukuliwa katika robo ya kwanza hadi ya Tatu ya mwaka huu wa fedha tayari imerudishwa na kwamba pamoja na unafuu wa masharti yake, bado kuna baadhi ya vikundi vinasuasua katika kuteresha mikopo hiyo.

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba, alitoa wito kwa wanufaika wa mikopo hiyo kujenga tabia ya kuirejesha kwa wakati ili iweze kunufaisha vikundi vingi zaidi kama inavyotarajiwa.

“Nyinyi leo mnanufaika na mikopo hii kwa vile kuna wenzenu waliofanya ustaarabu wakairudisha mikopo waliyokopa kwa wakati, nanyi hamna budi kuirudisha mikopo yenu kwa wakati ili inufaishe wengine wengi zaidi”,alisema.

Awali, mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Michael Mwandezi, alisema jumla ya shilingi milioni 100 zimetengwa katika robo ya nne ya mwaka fedha wa 2017/2018 kwa ajili ya mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana manispaa ya Moshi.

“Mikopo hii ni utekelezaji wa sera ya serikali  inayozitaka kila Halmashauri nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani  kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na walemavu”, alisema na kuongeza wanufaika wote wanatakiwa kuirejesha mikopo hiyo kwa wakati kwa vile si zawadi na kwamba mikopo hiyo iko kisheria kama ilivyo mikopo mingine hivyo masharti yote ni lazima yazingatiwe.

Wakizungumza baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo, walisema, imewasaidia kuanzisha miradi ya maendeleo na kujiajiri wenyewe, hatua ambayo imewawezesha kujikwamua kiuchumi na kuondokana na hali ya utegemezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi