• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

WANAWAKE NA VIJANA WAENDELEA KUNUFAIKA NA MIKOPO ISIYO NA RIBA

Posted on: March 27th, 2019

Halmashauri ya manispaa ya Moshi,imetoa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya shilingi milioni 225 kwa vikundi 45 vikiwemo vikundi 38 vya wanawake, 5 vya vijana na vikundi 2 walemavu, katika manispaa katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2018/2019.

Hayo yameelezwa na mkuu wa Idara Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii  Rose Minja, wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya Ths million 97  kwa ajili ya mikopo hiyo kwa vikundi 16 vya wanawake vikundi 3 vya vijana kwa robo ya tatu  ya mwaka wa fedha 2018/2019.

Katika hafla hiyo iliyofanyika  kwenye ukumbi wa Halamshauri, Minja alisema zoezi  utoaji wa mikopo hii isiyo na riba limezingatia masharti ya utoaji wa mikipo ambapo vikundi vyote ni lazima viombe mikopo kupitia kata husika na kuhakikisha vinatambuliwa na kata hiyo.Vile vile Idara inaangalia historia ya kikundi husika kujiridhisha uendeshaji wa kukundi hichi(VICOBA) kama kina uwezi wa kukopa na kurejesha. Licha ya kuwepo kwa mwitikio mkubwa wa vikundi kujitokeza na kuomba mikopo lakini vijana wameonekana kukosa muamko wa kujiunga katika vikundi na kupelekea kukosa fursa ya kupatiwa mikopo.

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba, alitoa wito kwa wanufaika wa mikopo hiyo kuhakikisha kuwa fedha wanayopewa inakwenda kutekeleza miradi /biashara walizokusidia na kujenga tabia ya kuzirejesha kwa wakati ili  ziweze kunufaisha vikundi vingi zaidi kama inavyotarajiwa.

“Nyinyi leo mnanufaika na mikopo hii isiyo na riba inayotolewa na serikali na mnayo nafasi kubwa ya kujikwamua kiuchumi na kuzisaidia familia zenu pamoja na kuhakikisha kuwa Manispaa na Wilaya yetu ya Moshi inakuwa  kiuchumi.Tunategemea baada ya muda mfupi mtakuwa kiuchumi na sisi tutahikisha tunawaunganisha na taasisi kubwa za kifedha ili muweze kukopa fedha zaidi .”,alisema na kuongeza tunaona kina mama mmekuwa mstari wa mbele katika kujitokeza kuomba mikopo naomba muwasaidia na vijana wenu ili waweze kujikwamua kiuchumi nao wahimizeni wajiunge kwenye vikundi kwa ajili ya kuwa na sifa ya kukopesheka.

Awali, Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Danfrod Kamenya, alisema Manispaa imeendelea kuhamasisha wanawake,Vijana na Walemavu kujiunga katika vikundi ili kupata fursa ya kupata mikopo isiyo na riba kutokana na asilimia kumi inayotengwa na Halmashauri kila mwaka kutokona na mapato ya ndani lakini tatizo limekuwa kubwa hasa kwa vijana wa kiume kutokuwa na muamko wa kufanya kazi katika vikudi. Hata hivyo Manispaa kwa kushirikiana na wadau inaendelea kuhamasisha vijana wa kiume wajiunge kweny vikundi na kufanya kazi kwa kushirikiana.

 Hatibu Hamad kutoka kwenye moja ya vikundi vya vijana vilivyonufaika na mkopo anasema vijana wengi wamekuwa wakikosa sifa ya kupatiwa mikopo kutokana na kutopenda kujiunga katika vikundi, huku wengi wakiwa hawana makazi maalumu.

Nao wanufaika wa mikopo hiyo wameishuruku Serikali ya awamu ya tano inayongozwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. John  P. Magufuli kwa kuwajali na  kuwawezesha wananchi hali ya chini hasa wajasiriamali wadogo kutoka kwenye vikundi(VICOBA)  kwa kuwapatia mikopo isiyo na riba na wameahidi kuitumia mikopo hiyo vizuri ili kutimiza lengo la serikali la kuwakwamua kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi