• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

WENYE ULEMAVU,WANAWAKE NA VIJANA WANUFAIKA NA MIK0PO ISIYO NA RIBA MANISPAA YA MOSHI

Posted on: January 18th, 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,imetoa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya shilingi milioni 100 kwa vikundi 18 vikiwemo vikundi 9 vya wanawake,7 vya vijana na vikundi 2 wenye ulemavu, Manispaa katika kipindi cha robo ya kwanza  ya mwaka  2019/2020.

Hayo yameelezwa na mkuu wa Idara Maendeleo ya Jamii  Rose Minja, wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya Ths million 100  kwa ajili ya mikopo hiyo kwa vikundi 18 vya wanawake,Vijana na  wenye ulemavu.

Katika hafla hiyo iliyofanyika  kwenye ukumbi wa Halmshauri, Minja alisema zoezi  utoaji wa mikopo hii isiyo na riba limezingatia sheria ya Fedha ya serikali za Mitaa sura 290. Na kanuni za utoaji na usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake ,Vijana na Watu wenye Ulemavu kifungu 37A (4) za mwaka 2019 na kanuni zake iliyotangazwa katika gazeti la Serikali Na.286 la tarehe 5/4/2019.

“Sifa za kupata mkopo ni kuwa vikundi vya Wanawake idadi ya wanakikundi wawe 10 na kuendelea,Vijana kinatakiwa  kiwe na Vijana 10 na watu wenye Ulemavu wanatakiwa wasio chini ya watu 5.Vikundi hivi havitajumuisha wajumbe wenye ajira rasmi na wanatakiwa wawe na mradi wa pamoja”.Alisema Rose

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba, alitoa wito kwa wanufaika wa mikopo hiyo kuwa kuhakikisha kuwa kama wanaona mambo sio mazuri katika uendeshaji wa mradi waliochagua wanatakiwa wasisite kuomba ushauri kwa wataalamu wa Manispaa kama vile Afisa biashara na Mchumi ili kuhakikisha wanafanikiwa malengo waliojiwekea.

“Sina wasiwasi na wakinamama kwani huwa wanaambizana wakati wanaona mambo hayaendi vizuri au mmoja wao anawakwamisha lakini kwa Vijana jambo hilo  mara nyingi huwa halifanyiki.Nawasihi Vijana kuhakikisha kuwa mnakwenda pamoja katika uendeshaji wa miradi na mtumie muda wenu mwingi kushirikiana na kukumbushana ili mfanikiwe kwa pamoja”.,alisema na kuongeza  Vijana tushikamane pamoja ili tufanikiwe na kufanikisha mlichokusudia ili kuonyesha shukrani kwa Serikali  ya CCM  na awamu Tano kuwa imewajali na imewakwamua  kwa kuwapa mikopo hii isiyokuwa na riba.

Awali, Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Lainie Kamendu, alisema Manispaa imeendelea kuhamasisha wanawake,Vijana na Walemavu kujiunga katika vikundi ili kupata fursa ya kupata mikopo isiyo na riba kutokana na asilimia kumi inayotengwa na Halmashauri kila mwaka kutokona na mapato ya ndani robo ya pili Halmashauri inayo  kiasi cha Tsh.  Milion 300 ila kwa  siku hii ya leo tunatoa mikopo yenye thamani ya Tsh million 100 na baada  ya wiki mbili mchakato mwingine utakuwa umekamilika na tunatarajia kutoa mikopo mingine yenye thamni ya Tsh. Million 200.

Nao wanufaika wa mikopo hiyo wameishuruku Serikali ya awamu ya tano inayongozwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. John  P. Magufuli kwa kuwajali na kutunga sheria  iliyoboresha utoaji wa mikopo kwa Wajasiriamali wadogo wenye mradi mmoja .Kwasasa sisi tunamradi mmoja tunaoundesha kwa pamoaj hivyo ni rahisi sisi kurejesha mkopo kwani tunafanya kazi pamoja na sio kama mwanzo tulikuwa chukua fedha kama kikundi na kila mmoja anafanya shughuli yake na kuleta shida wakati wa marejesho.



Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi