• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

VIKUNDI 378 VYANUFAIKA NA MIKOPO WA ZAIDI YA TSH. BILIONI 2.1

Posted on: March 8th, 2021

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imetoa mikopo ya kiasi cha Tsh. 2,101,740,000 katika kipindi cha mwaka 2015 hadi Machi 2021 ikiwa ni azma ya utekelezaji wa agizo la serikali la kuzitaka kila Halmashauri  kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato yake ya ndani  kwa ajili ya kutuo mikopo ya kuwawezesha Wanawake,Vijana na Walemavu.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi. Rose Minja  ameeleza kuwa mikopo hiyo imetolewa kwa vikundi vya wajasiriamali wa Manispaa ya Moshi ambapo Vikundi 292 vya wanawake vimepata Ths 1,549,502,000, Vikundi vya vijana 79 vimepewa Ths 523,322,000 na vikundi vya watu wenye ulemavu  7 vimepata kiasi cha Ths 29,000,000.

Bi Rose Minja ameeleza hayo wakati wa  kukabidhi Mikopo ya kiasi cha Tsh 295,290,000 zilizokopeshwa kwa Vikundi 47 vikiwemo 31 vya wanawake na 16 vya vijana kwenye  Maadhimisho Siku ya Wanawake Duniani  iliyofanyika  kwenye Viwanja vya Uhuru Park Manispaa Moshi  

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Alhaji Rajab Kundya amewaasa wanavikundi waliopewa mikopo hiyo kutumia fedha hizo katika shughuli mbalimbali za kiuchumi walizokusudia kufanya na si vinginevyo.

“Ninawaomba muache kufikiri kuwa fedha hizo mnapewa kama zawadi ambazo mnaweza kuzitumia mnavyopenda, bali mnatakiwa kuzitumia fedha hizo kwa shughuli za kiuchumi zilizokusudiwa na kuzirejesha kwa wakati ili ziweze kukopeshwa kwa vikundi vingine”Alisema Alhaji Rajabu  Kundya

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Juma Raibu Juma ameeleza kuwa Halmshauri itahakikisha  itatimiza matakwa ya sheria kwa kuwakopesha asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa mwaka huu wa fedha 2020/2021.

“Hata kama tuna changamoto nyingi tutahakikisha tunaendelea kutoa mikopo hii  na  tunawaomba msituangushe kwani sisi tunatimiza wajibu wetu na nyie mtimize wajibu wenu wa kutumia fedha hizi vizuri kwa ajili ya maendeleo yenu na kuzirejesha ili zoezi hili la kukopesha vikundi liwe endelevu “Alisema Mstahiki Meya

Bi Emeresiana Shirima anaishukuru Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mh Rais Dr John Joseph Magufuli kwa kuwajali na kuwapa  mikopo isiyo na riba na yenye masharti nafuu  ambayo itatuwezesha kutuinua kiuchumi na tunaahidi tutahakikisha kuwa tutarejesha kama ilivyo kwenye mikataba.  



Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi