• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UZINDUZI WA MAJUKWAA YA WANAWAKE KIUCHUMI

Posted on: October 31st, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imezindua rasmi majukwaa ya kuwawezesha wanawake kiuchumi katika ngazi ya Kata ikiwa ni moja ya malengo yake ya kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Katika kutekeleza mpango wake Manispaa ya Moshi imeanzisha na kuzindua majukwaa tisa kwenye kata za Rau,Mfumuni, Karanga,Msaranga,Pasua, Bomambuzi, Majengo, Mimbeni,na njoro ambapo lengo kuu ni kuanzisha majukwaa katika kata zoete 21 za Manispaa hadi kufikia mwezi novemba mwaka huu.

Akizindua majukwaa hayo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii  Manispaa ya Moshi, Rose Minja alisema zaidi wanawake  6000 watanufaika na mpango huo wenye lengo la kuleta mwanga mpya kwa wanawake pamoja na kutumia ujuzi walionao kujikwamua kiuchumi.

Alisema malengo mengine ya kuanzishwa kwa majukwaa ya wanawake ni kuwaunganisha wanawake katika ngazi zote ili waweze kuwa na uelewa juu ya masuala mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa masoko,uibuaji wa fursa,shughuli za ujasiaramali,fursa za mikopo,pamoja na kupeana uzoefu katika uendeshaji wa vikundi kama VICOBA na SACCOS.

Katika hatua nyingine, Rose alisema ili wanawake waweza kujikwamua kiuchumi ni lazima wawe mstari wa mbele kupinga  mila potofu na kandamizi ambazo zimepitwa na wakati kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya  kijamii na kiuchumi.

 “Katika kufanikiwa haya yote ni lazima wanawake wajitambue, wawe tayari kukubali mabadiliko,wapendane, waweze kujua mahitaji yaliyopo sokoni, waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa pamoja na kufanya ushindani wenye tija”Alisema  Rose.

Ili kuweza kufanikisha malengo yake Manispaa ya Moshi inashirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali na  wadau mbalimbali katika utekelezaji wa mpango huo.

Miongoni mwa mashirika yanayoshirikiana na Mansipaa ya Moshi ni shirika la kuhudumia viwanda vidogo SIDO,pamoja na taasisi za kifedha kwa ajili ya kutoa elimu kuhusiana na masuala ya ujasiriamali,utafutaji wa masoko,uanzishwaji wa viwanda vidogo,pamoja na kuwaunganisha wajasiriamali na mamlaka ya chakula na dawa TFDA pamoja na mamlaka ya viwango nchini TBS.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi