• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

SHIRIMATUNDA WAMSHUKURU DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Posted on: November 7th, 2023

WANANCHI wa Kata ya Shirimatunda Manispaa ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro wameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi Millioni 500 zilizopelekea uboreshaji wa miundombinu ya zahanati ya Shirimatunda, iliyoko kwenye Kata hiyo.

Akitoa pongezi hizo kwa niaba ya wananchi hao, Diwani wa Kata ya Shirimatunda Bw. Francis Shio amesema kuwa maboresho hayo ni faraja kubwa kwa wananchi wa Kata hiyo na zingine za jirani zikiwemo za wilaya za jirani.

“Maboresho ya miundombinu yaliyofanywa na Serikali katika zahanati hii ni sehemu ya huduma za Serikali ambazo zimewanuwaisha na zimewaridhisha wananchi wa Kata yetu na wale wa Kata za jirani”, amesema Mhe Shio.

Amesema kuwa mbali na wakazi wa Kata ya Shirimatunda, pia zahanati hiyo inawahudumia wananchi wa wilaya ya Hai katika vijiji vya Shirimatunda (Hai), Shirimgungani (Hai) na Mijengweni (Hai) na kijiji cha Chekereni katika wilaya ya Moshi.

Mhe. Shio aliendelea kusema kuwa kwa upande wa manispaa ya Moshi, zahanati hiyo inawahudumia wananchi wa Kata za Soweto, Karanga na Shirimatunda yenyewe.

“Nichukue nafasi hii kwa niaba ya wananchi kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha hizi za ujenzi na kwa maono na mawazo yake chanya yanayolenga kuboresha sekta ya afya hapa nchini ikiwemo kuleta wataalam wa afya, kwani yanajibu kero za wananchi kwa vitendo”, amesema Diwani Shio

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi kati zahanati hiyo Dkt. Edna Silayo, amesema maboresho ya miundombinu katika zahanati hiyo yamesaidia kuongeza ari ya watumishi katika zahanati hiyo.

“Jumla ya shilingi Millioni 500 zilizotolewa na Serikali zimewezesha ujenzi Jengo la wagonjwa wanje, Jengo la Maabara, Jengo la kufulia,Jengo la Mama na mtoto na chumba cha upasuaji, pamoja na njia za kutembelea kwa miguu na Kichomea taka cha kisasa hali hii imechangia kuongeza ari ya watumishi kwani hata nafasi za kutolea huduma zimeongezeka”, alisema.

Amesema kabla ya hapo wafanyakazi walikuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu kutokana na ufinyu wa nafasi ambayo ilikuwa inasababishwa na ufinyu wa majengo ya kutolea huduma.

“Tulikuwa hatuna maabara nzuri wala jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje, badala yake huduma hizi zilikuwa tunazitolea kwenye chumba kimoja kwa kila idara”, amesema Dkt Silayo

Aliendelea kusema kwa baada ya ujenzi wa jengo la OPD na maabara kukamilika, jengo la zamani la OPD kwa sasa linatumika kwa ajili ya huduma za wazazi (Kliniki ya wajawazito) pamoja na huduma za wale wenye upungufu wa kinga mwilini.

“Maboresho haya hayajawanufaisha wahudumu wa afya tu bali pia wananchi ambapo wale wanaofuatilia huduma tunazotoa hapa idadi yao imeongezeka kutoka wastani wa kati ya watu 20 hadi 25 kwa siku na kufikia wastani wa watu kati ya 25 hadi 40 kwa siku”, Dkt Silayo amesema.

“Kwa sasa wigo wa maeneo ya kutolea huduma umeongezeka kutokana na Serikali kutoa fedha ziliziopelekea ujenzi wa majengo haya ya ziada na ndiyo maana watu wanaamua kufuata huduma hapa ambapo ni karibu na maeneo wanayoishi”, a.

Mmoja wa wananchi wa eneo hilo Bi Liana Ndanshau ameipongeza Serikali kwa maboresho hayo ambayo amesema yamewasaidia kupata huduma muhimu na kwa haraka haswa nyakati za jioni au usiku.

“Tulikuwa tunapata wakati mgumu pale mtu unapokuwa na dharura ya ugonjwa au hata mwenzako au jirani ambaye ni mgonjwa, ilikuwa inatulazimu kutafuta njia za haraka kufuata huduma nje ya hapa lakini kwa maboresho haya, hayo yatakuwa ni historia”, Amesema Bi Liana

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi