• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

SERIKALI KUU HAINGILII MAAMUZI YA BARAZA LA MADIWANI

Posted on: October 6th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Saidi Mtanda ameeleza kuwa sababu zinazosababisha Serikali kuu kuingilia maamuzi ambayo yamekuwa yakifanywa na baraza la madiwani ni pamoja na uwepo wa maamuzi ya baraza la madiwani yasiyofuata Katiba, Sera za Kitaifa,Sheria, Kanuni  na miongozo inayotolewa na Serikali.

Mtanda ametoa kauli hiyo wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo  Waheshimiwa Madiwani  na Wakuu wa idara wa Manispaa ya Moshi kuhusu masuala mbalimbali ya kiutendaji ikiwemo misingi ya maadili ya viongozi wa umma, majukumu ya waheshimiwa madiwani, usimamizi wa Rasilimali fedha katika serikali za mitaa,Mahusiano ya madiwani na watendaji na uhusiano kati ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.

“Sisi tunapojiridhisha kwamba baraza linatekeleza wajibu wake kwa kufuata Katiba ya Nchi, Sheria, na kanuni na kufuata huwa hatuna maneno na nyie lakini baraza mkifanya maamuzi kinyume na utaratibu huwa  tunatoa maelezo na ushauri wa namna ya kufanya ili mambo yaenda sawasawa”Alisema Mtanda.

Mtanda alisisitiza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ipo tayari wakati wowote kushirikiana na Waheshimiwa Madiwani na Serikali kuu huwa haina tabia ya kuingilia maamuzi ya baraza la madiwani bali kinachofanyika ni kushauri ili kuhakikisha kunakuwepo na utawala bora unaofuta sheria za nchi.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Juma Raibu amesema mafunzo hayo yatawawezesha madiwani na watendaji kushirikianza kwa karibu katika kutekeleza  majukumu yao kwa mujibu wa sheria kwa lengo la kuwaletea wananchi wa Manispaa ya Moshi Maendeleo.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya sisi Madiwani wa Manispaa ya Moshi tunashirikiana vizuri na Watendaji na hakuna mgogoro wowote kwani tunafanya kazi kwa kushirikiana na kuheshimiana “.Alisema Raibu.

Mstahiki Meya ameeleza kuwa mafunzo haya yatakuwa chachu kwao katika kuendesha Halmashauri kwani kwa sasa Waheshimiwa madiwani wameongeza elimu kwa kujua majukumu yao hasa katika kusimamia Rasimali fedha na mahusiano kati ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi