• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MSTAHIKI MEYA WA TUBINGEN ARIDHISHWA NA UENDESHAJI WA KIWANDA CHA MBOJI

Posted on: May 12th, 2022

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imefanikiwa kupata kiasi cha Tsh Milioni 42 kama mapato ya ndani baadaya ya kuzalisha na kuuza tani 157 za mbolea ya mboji kwenye kiwanda chake kilichopo eneo la Mtakuja katika kipindi cha Desemba 2020 na Aprili 2022.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Idara ya usafi na mazingira  Bi Viane Kombe wakati akiwasilisha taarifa ya mradi huo katika ukumbi wa Manispaa kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Tubingen  nchini Ujerumani Bw Boris Palmer,  na madiwani kutoka Tubingen walipotembelea hamashauri ya Manispaa ya Moshi.

“Mradi huu mbali na kuiingizia halmashauri mapato, pia umechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha mazingira wilaya ya Manispaa ya Moshi kwa ujumla kutokana kuwa unatumia malighafi ambazo ni taka zinazozalishwa kufuatia matumizi ya matunda na mbogamboga”, alisema Bi Viane

“Jumla ya tani 236 za taka ngumu huzalishwa Manispaa ya kila siku ambapo katika kipindi hicho cha mwaka mmoja jumla ya tani 2,058 za mbogamboga na matunda zilitumika kuzalisha mbolea ya mboji kupitia mradi huu”, alisema.

Bi Kombe aliendelea kueleza kuwa katika kufannya mradi huo kuwa endelevu, baadhi ya mikakati imekuwa ikitekelezwa ikiwemo kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi ili kujenga kizazi kijacho kitakachokuwa na uelewa mpana wa utunzaji wa mazingira.

“Wanafunzi katika Vilabu 45 mazingira kutoka shule 20 za msingi  wamepatiwa mafunzo kuhusu  kutengeneza mbolea ya mboji na kutenganisha taka ngumu ambazo ni malighafi ya kutengenezea  mbolea ya mboji”, alisema.

Kupitia mradi huu wanafunzi wamepata elimu pamoja na kushirikishwa katika zoezi la  kupanda miti na kuitunza kwa kutumia mbolea ya mboji  katika maeneo ya shule.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Meya wa Jiji la Tubingen Mhe. Boris Palmer alielezea kuridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao unaendeshwa kupitia ufadhili wa Jiji hilo kwa kushirikiana na Manispaa ya Moshi kutokana na undugu ulioko kati ya Jiji la Tibingen na Manispaa ya Moshi.

“Ni furaha kwangu mimi kuona ya kuwa mradi huu umelepata mafanikio makubwa, haswa ikitiliwa maanani nilikuja hapa mwaka wa 2010 kwa ajili ya kuanza mikakati ya kuuanzisha”, alisema Palmer

Aliongeza, “Mradi huu ni kielelezo tosha ya jinsi watu kutoka nchi mbili tofauti tena kutoka mabara mawili tofauti wanavyoweza kushirikiana kupitia halmashauri zao kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa watu wote tena kwa mafanikio makubwa”.

“Mbali na mradi huu pia tumejenga mahusiano mazuri kati yetu ambapo kwa sasa kahawa inayotoka mkoani Kilimanjaro inauzwa katika Jiji la Tubingen na hivyo kuwaingizia mapato wakulima wa kahawa na mapato na Taifa”, alisema.

Kwa upande wake Kaimu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mhe Stuart Nkinda alipongeza uongozi na wananchi wa Jiji la Tubingen kwa ushirikiano walioutoa katika kufanikisha mradi huu ambao alisema mbali na kuboresha mazingira na kuingiza mapato pia umechangia kupatikana kwa ajira kwa wakazi wa Manispaa ya Moshi.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi