• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA YA MOSHI AWATEMBELEA WANUFAIKA WA TASAF

Posted on: March 14th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba, amewataka wanufaika wa Mfuko wa maendeleo ya Jamii (Tasaf) mpango wa kunusuru kaya maskini, Manispaa ya Moshi,Mkoani Kilimanjaro kutumia fedha wanazozipata, kuanzisha miradi midogomidogo ambayo itawawezesha kujikwamua  kiuchumi.

Warioba alisema hayo wakati alipotembelea baadhi ya wanufaika hao,pamoja na kutoa elimu ya awali kabla ya kupewa fedha na kushuhudia walengwa hao walivyonufaika na fedha ambazo wamekuwa wakipewa kwa kuanzisha miradi.

Alisema wapo wanufaika wa Tasaf ambao wametumia fedha walizozipata kuanzisha miradi na kuweza kupiga hatua ya kimaendeleo, hivyo ni vyema wanufaika wote wakaiga mfano huo ili kuweza kuondoka kwenye kundi la kusaidiwa na kuachia wengine kufikiwa.

“Mchango mdogo wa Tasaf mnaoupata utumieni vizuri, msikate tamaa na kubweteka,anzisheni miradi midogo midogo ya maendeleo, ili kuweza
kujiinua kiuchumi, kwani tunategemea baada ya muda msimame wenyewe na
kuendesha maisha yenu bila kutegemea msaada wowote”alisema Warioba.
Akizungumza Mratibu wa mpango wa kunusuru Kaya Maskini Manispaa ya Moshi, Dennis Robert,alisema jumla ya fedha ambazo zimewafikia walengwa 1,461wa mpango huo mpaka sasa ni Sh 1.5 Bilioni katika mizunguko 22.
Alisema mpaka sasa walengwa zaidi ya 200 wameanzisha miradi ya ufugaji wa kuku,bata ,mbuzi na kuanzisha biashara ndogondogo,huku wengine 300 wakijiingiza kwenye kilimo,hatua ambayo imewawezesha kubadilisha maisha yao na kuondoka kwenye mlo mmoja waliokuwa wakiupata na sasa kupata milo mitatu kwa siku.

“Wapo baadhi ya Walengwa wa mpango wa kuzinusuru kaya Maskini,ambao wamepiga hatua kupitia fedha kidogo wanazozipata, wameanzisha miradi na kwa sasa wanapata chakula bila shida, wanasomesha watoto wao na wamewakatia bima za afya, lakini pia ipo changamoto ya uwepo wa watu maskini ambao bado hawajafikiwa”alisema.

Baadhi ya walengwa walisema kupitia fedha kidogo wanazozipata kutoka Tasaf, wameweza kuanzisha miradi ya ufugaji na biashara ndogondogo na kwa sasa wameweza kupiga hatua ya kimaendeleo na hata kununua kiwanja na wengine kuanza ujenzi.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi