• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA YA MOSHI AUPONGEZA UONGOZI WA MANISPAA KWA KUTOA MIKOPO YA SHS. 367,550,000.

Posted on: November 10th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe. Abbas Kayanda ameupongeza Uongozi na Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa kutimiza takwa la kisheria inazozitaka Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuvikopesha Vikundi vya Wanawake, Vijana na watu Wenye Ulemavu.

Kayanda ametoa pongezi hizo wakati akikabidhi mfano wa hundi ya  mikopo isiyo na riba kiasi cha Shs.  367,550,000 ambazo zinakopeshwa kwa vikundi 61. Vikundi 42 vya Wanawake vimekopeshwa sh.240,500,000, vikundi 15 vya Vijana vimekopeshwa  kiasi cha Shs.119,050,000  na vikundi 4 vya Watu wenye Ulemavu vimekopeshwa kiasi cha Shs 8,000,000. 

“Leo ninyi mnanufaika na mikopo hii kwa vile kuna wenzenu waliokopeshwa kipindi kilichopita na wakazitumia kwa malengo yaliyokusudiwa  kisha wakairudisha mikopo yao kwa wakati, nanyi hamna budi kuirudisha mikopo yenu kwa wakati ili iweze kuja  kuwanufaisha wengine wengi zaidi”,alisema.

  Amewataka wote waliopokea mikopo kuhakikisha inawanufaisha katika shughuli za kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kukua kutoka hatua moja Kwenda nyingine.

“Tunategemea kama kikundi kilikopa kiasi kidogo kifanye shughuli zake vizuri na kurejesha ili kipindi kijacho kiweze kukopeshwa fedha zaidi na kukuza biashara hata kuweza kufungua kiwanda”

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi  Mhandisi Zuberi Kidumo  alisema  kuwa Mikopo hii ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020/2025 na  Sera ya serikali inayozitaka kila Halmashauri nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya mikopo ya Wanawake, Vijana na  Watu wenye Ulemavu.

“ Tunawaomba wanufaika wote mtambue kuwa mikopo hii ipo kisheria na sio zawadi hivyo mnatakiwa kuitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa ili muweze kurejesha kama sheria inavyotaka” Alisema

Awali Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Bw. Denis Shette alisema Katika mwaka wa fedha 2021/2022 robo ya kwanza hadi ya tatu Halmashauri ilifanikiwa kukopesha vikundi 159  kiasi cha sh.949,398,700 ambapo vikundi 116 vilikuwa vya wanawake,32 vya vijana na 11 vya watu wenye ulemavu.

Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI SHULE YA SEKONDARI MAWENZI July 27, 2022
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • WANANCHI WA KATA YA MSARANGA WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUWAJENGEA SHULE YA SEKONDARI

    February 22, 2023
  • ZAIDI YA BILIONI 50.1 KUTUMIKA MANISPAA YA MOSHI 2023/2024

    February 14, 2023
  • MKUU WA WILAYA AWAPONGEZA WALIMU WA MANISPAA YA MOSHI

    January 10, 2023
  • MKUU WA WILAYA YA MOSHI AUPONGEZA UONGOZI WA MANISPAA KWA KUTOA MIKOPO YA SHS. 367,550,000.

    November 10, 2022
  • Tazama

video

LISHE KUWA AJENDA YA KUDUMU MANISPAA YA MOSHI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi