• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA AWAPONGEZA WALIMU WA MANISPAA YA MOSHI

Posted on: January 10th, 2023

MKUU wa wilaya ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro, Mhe. Abbas Kayanda, amewapongeza walimu na uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa kazi nzuri na juhudi kubwa walizozifanya katika sekta ya elimu zilizopelekea Manispaa ya Moshi kufanya vizuri kwenye matokeo ya Mtihani wa  Kitaifa wa kumaliza Elimu ya msingi

Kayanda alitoa pongezi hizo baada ya kupokea taarifa ya elimu kwa mwaka wa 2022 iliyotolewa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Rashid Gembe, katika kikao cha Maafisa Elimu, Waratibu Elimu Kata na Watendaji wa kata kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro.

“Ufaulu katika mitihani ya Shule za Msingi kwa Manispaa ya Moshi katika miaka ya hivi karibuni umeipa wilaya ya Moshi heshima ya kipekee katika Mkoa wa Kilimanjaro, ombi langu kwenu msibweteke na mafanikio haya badala yake mzidishe juhudi ili mafanikio haya yafikie ngazi ya Taifa”, alisema.

Mhe.Kayanda alisema kuwa Manispaa ya Moshi imekuwa ikifanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa ya Darasa la Saba katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, huku asilimia ya ufaulu ikiongezeka kitaifa na kimkoa kila mwaka.

“Taarifa za kitaifa zinazohusiana na matokeo ya mitihani ya Darasa la Saba yanaonyesha kuwa Manispaa ya Moshi imeshika nafasi ya tano kitaifa mwaka wa 2020, nafasi ya tatu mwaka wa 2021 na nafasi ya pili mwaka 2022, haya ni mafanikio makubwa ya kujivunia”, alisema.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Bw Rashid Gembe alisema mafanikio hayo yametokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na Manispaa pamoja na walimu .

“Wanafunzi hupata chakula cha mchana kutokana na mpango wa  wazazi kuchangia chakula baada ya kupata kibali maalum cha kuchangia chakula kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya”, alisema na kuongeza kwa uchangiaji chakula cha mchana shuleni umechochea kuongeza kiwango cha taaluma miongoni wa wanafunzi wa Shule za Msingi.

Alisema sababu nyingine ni ile ya uboreshaji wa miundombinu ya shule ambapo katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Manispaa ya Moshi kupitia mapato ya ndani ilitoa  jumla ya shilingi milioni 400 zilizotumika kuboresha miundombinu katika Shule za Msingi.

“Katika maboresho hayo, vyoo 60 vimejengwa sambamba na madarasa 11 mapya na mengine mawili yalifanyiwa ukarabati mkubwa; marekebisho haya pia yamechangia kuboresha miundombainu inayotosheleza kupokea wanafunzi wa Darasa la Awali na Darasa la Kwanza mwaka 2023”, alisema.

Aidha alisema hadi kufikia Juni 30, 2022, kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jumla ya shilingi 417,359,646.08 zilipokelewa shuleni ikiwa ni Ruzuku ya Elimu Msingi Bila Ada (EMBA) kwa ajili ya maendeleo ya elimu shule za msingi, ambapo alisema kiasi hicho ni sawa na asilimia 97.3 ya kiasi cha 428,874,000 ya fedha zote za EMBA, ambazo ziko kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2022/2023

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi