• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA AAGIZA MANISPAA KUTENGA BAJETI YA KUTOSHA KWA SHUGHULI ZA LISHE

Posted on: November 28th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kisare Makori, ameuagiza Uongozi wa Halmshauri Manispaa ya Moshi kuhakikisha unatenga bajeti ya kutosha kulingana na maelekezo ili kusaidia juhudi katika kuboresha huduma za lishe kwa wananchi na kufanikisha mapambano dhidi ya utapiamlo.

Kisare ametoa Rai hiyo leo wakati akifungua kikao cha maandalizi ya mpango na Bajeti ya Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo amesema Manispaa ya Moshi inatakiwa kuhakikisha Bajeti itayotengwa   mwaka huu inakidhi vigezo na inazingatia maoni yalitolewa na wadau katika vikao vya tathmini ya lishe ya Manispaa ya Moshi.

“Tunatambua kuwa lishe duni huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili, hivyo kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na Taifa hivyo ni wajibu wetu kutenga bajeti ya kutosha kwa shughuli za Lishe ili tuweze kukabiliana na tatizo la lishe duni na Utapiamlo “Alisema Kisare

Aliendelea kueleza kuwa  pamoja na maendeleo ambayo nchi hii imekuwa ikiyapata katika maeneo mbalimbali, bado utapiamlo umeendelea kuathiri jamii, hivyo uboreshaji wa hali ya lishe Nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na kupunguza umaskini kwa mtu mmoja mmoja na Nchi kwa ujumla.

"Matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata kuua watoto na wanawake hasa wajawazito na wanaonyonyesha, naomba tuongoze juhudi katika kuboresha shughuli za lishe kwa jamii ya wananchi wa Manispaa ya Moshi,kwani jamii inategemea sana uongozi wetu katika kusimamia vyema mapambano dhidi ya utapiamlo”Alisema

Aidha, Alisema kuwa naamini tukitenga bajeti yenye kutosheleza kwa shughuli za lishe na kuwajibika ipasavyo itasaidia kuimarisha hali ya lishe na kupunguza tatizo la utapiamlo na kusababisha kufikiwa kwa malengo ya maendeleo katika nchi yetu,

Vile Vile ameutaka uongozi wa Manispaa kuhakikisha kuwa fedha za lishe zinatengwa na kutolewa kwa wakati kulingana na bajeti ili kuwezesha shughuli zinazohusiana na lishe kutekelezwa kwa wakati na kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi