• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AWATAKA WALIOPEWA DHAMANA YA KAZI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Posted on: August 21st, 2022

MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw Nurdin Babu, amewataka wale wote waliopewa majukumu ya kuendesha zoezi la Sensa ya watu na Makazi kutekeleza wajibu wao ipasavyo ili kukamilisha kazi nzuri aliyoifanya Rais Samia Hassan ya kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi hilo.

Bw Babu alitoa wito huo  wakati alipopokea taarifa ya matayarisho ya zoezi hilo kwa manispaa ya Moshi kwenye kikao cha pamoja  kilichofanyika katika ukumbi wa CCM Mkoa.

"Sensa ya watu na makazi ni muhimu kwa Taifa kwa ajili ya Serikali kupanga mipango ya maendeleo; ni kutokana na umuhimu huo Rais Samia alitumia muda mwingi kuhamasisha kuhusiana na zoezi hili kupitia hotuba zake mbalimbali; tukifanikisha zoezi hili tutakuwa tumekamilisha kazi nzuri  aliyoifanya", alisema.

Aidha aliwataka wananchi kutokuwa na hofu na maswali yatakayoulizwa kutokana na madodoso yaliyotayarishwa kwa ajili ya zoezi hili na kwamba wanachotakiwa ni kujibu yale ambayo yanawahusu tu.

"Utaulizwa kwa mfano una gari au nyumba na kadhalika; sasa usipate hofu kwamba maswali hayo ni ya nini, iwe unavyo hivyo vitu au la unachotakiwa ni kujibu ndiyo au la, unatakiwa  kujibu yale yanayokuhusu tu, majibu utakayotoa hayatakuathiri kwa njia yoyote ile", alisema.

Aidha alitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano wao wa dhati kwa wale waliopewa dhamana  ya  kuendesha zoezi hili  ili kulifanya iwe rahisi kwao na kwamba kufanikiwa kwake ni mwanzo wa Serikali kupanga mipango bora ya maendeleo ambayo itawahusu wananchi wenyewe.

Pia katika mkutano huo ambao uliwashirikisha viongozi wa mitaa, kata za manispaa ya Moshi alitoa wito kwa wananchi kutokuwaficha wenzao wenye kuishi na ulemavu wa aina yoyote kutokana na ukweli ya kuwa mipango ya maendeleo inawahusu na wao vilevile.

"Nyinyi mnawajua wale wote walioko maeneo yenu ya kiutawala, pale mtakapogundua kuna mtu anaeishi na ulemavu halafu jamaa zake wamemficha ili asihusishwe kwenye zoezi hili muhimu toeni taarifa haraka iwezekanavyo ", alisema.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa  amewataka viongozi hao wa Mitaa na wale wa Kata kujenga tabia ya kumsemea Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi nzuri anayoifanya kwa ajili ya Watanzania na Taifa lote kwa ujumla.

"Sisi kama viongozi tunajua kazi nzuri anazofanya Rais lakini si wote walio nje ya uongozi wanaojua hayo, hivyo ni wajibu wenu kila mnapokutana na wananchi huko kwenye maeneo yenu ya kazi mtangaze kazi nzuri zinazofanywa na Rais ili wawe na uelewa na kuepukana na maneno yanayoenezwa na wale wasio na nia njema kwa Serikali wanaosema hakuna kazi zinazofanyika", alisema

Awali akitoa taarifa ya maendeleo ya maandalizi ya zoezi la sensa ya watu na makazi, mratibu wa sensa ya watu na makazi manispaa ya Moshi Bi Lucia Raphael alisema hadi kufikia Agosti 20, 2022, mipango yote ilikuwa imekamilika kwa asilimia kubwa.

"Utengaji wa maeneo madogomadogo ya kijiografia 353 umefanyika na kukamilika katika mitaa yote 60 ndani ya kata zote 21 ndani ya Moshi Manispaa", alisema.

Aidha alisema makarani, wasimamizi maudhui 95, wasimamizi wa TEHAMA 21, makarani wa kawaida 798, makarani wakuu 60 na wakufunzi 54 wameshapatiwa mafunzo kupitia ngazi mbalimbali zikiwa za Wilaya na Mkoa.

"Mafunzo ya vitendo kwa makarani, wasimamizi wa maudhui na  TEHAMA yalifanyika kwa siku 19 na mazoezi ya vitendo kufanyika katika Kata za Rau, Korongoni, Soweto, Karanga, Longuo B na Bomambuzi", alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi