• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AMETANGAZA KUWA KILA SIKU YA JUMAMOSI ITAKUWA NI SIKU YA USAFI MANISPAA YA MOSHI

Posted on: October 8th, 2022

Mkuu wa Kilimanjaro, Nurdin Babu ametangaza kuwa kila siku ya Jumamosi itakuwa siku maalumu ya kufanya usafi kwa wakazi wa Manispaa ya Moshi.

Babu ametoa agizo hilo leo Jumamosi tarehe 8/10/22 kwenye uzinduzi wa zoezi la kufanya usafi lililofanyika katika soko na Mbuyuni na Manyema kata ya Bondeni Manispaa ya Moshi kwa lengo la kuwakumbusha wananchi wa Manispaa ya Moshi kuendelea na utamaduni wa kudumisha usafi na kutunza Mazingira.

“Natambua kuwa huwa mnafanya usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na leo hii nimezindua rasmi zoezi la kufanya usafi kila Jumamosi , hili ni agizo kwani tunataka kuendeleza heshima ya  Manispaa ya Moshi ya kuongoza kwa usafi nchini kila mwaka.Ni wajibu wa kila wananchi kushiriki zoezi hili kikamilifu na kuhakikisha kuwa sehemu anayokaa au kufanya shughuli zake za kiuchumi au kijamii inakuwa safi” Alisema

Aidha amewataka wananchi wote kuhakikisha kuwa kila Jumamosi hakuna kufungua biashara au ofisi kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 3 kamili kwani muda huu utakuwa ni muda wa kufanya usafi tu.

Mkuu wa Mkoa ameeleza  kuwa Serikali haitaki kugombana na watu hivyo anawaomba wananchi kuzingatia maagizo hayo kwani atakuwa anapita kila siku ya jumamosi akiwa na jeshi la akiba ili kukagua na kuangalia utekelezaji wa agizo lake.

Babu amesema katika siku hiyo, kila mmoja anapaswa kutekeleza wajibu wake kuanzia ngazi ya kaya, Mtaa na Kata na kuwataka wananchi kujumuika katika kufanya usafi.

Uzinduzi wa Zoezi hilo la usafi lililoongozwa na Mkuu wa Mkoa  liliwahusisha Mkuu Wilaya ya Moshi ,Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi , Mkurugenzi  wa Manispaa ,Waheshimiwa Madiwani, Jeshi la Zimamoto na Jeshi la Akiba, Uhamiaji, Jeshi la Polisi, Watendaji wa  Halmashauri na Mamlaka ya Maji Safi na Utunzaji wa Mazingira, Wafanyakazi kutoka Bonde la Mto Pangani, Benki ya NMB, Benki ya Mkombozi na wananchi.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi