• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MILA KANDAMIZI ZINAWANYIMA WANAWAKE FURSA

Posted on: March 8th, 2018

Imeelezwa kuwa,Mila kandamizi na mfumo dume uliopo katika jamii, ni changamoto inayowanyima wanawake fursa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kumiliki mali ikiwemo Ardhi.

Mbali na hilo,vitendo vya  kikatili, vinavyoendelea kushamiri  katika maeneo mbalimbali nchini,pia vimekuwa vikiwakandamiza wanawake katika kupata haki na kuwafanya kudharaulika katika jamii.

Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa Miradi katika asasi isiyo ya kiserikali ya Elimu Mwangaza Tanzania, Upendo Ramadhani,wakati akisoma taarifa kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, katika Manispaa ya Moshi .

Upendo alisema,pamoja na mafanikio ambayo wameyapata wanawake,bado wanakumbana na vikwazo mbalimbali ikiwemo mila na desturi kandamizi ambazo zinawanyima fursa ya kuwa viongozi katika ngazi za kutoa maamuzi, kwenye familia na hata kwenye jamii.

"Mila,Desturi na mfumo dume,bado ni changamoto kwa wanawake katika jamii nyingi nchini, na changamoto hii inawanyima wanawake haki ya kuzungumza kutoa maoni,kuwa viongozi na kumiliki mali ikiwemo Ardhi"alisema.

Katika hatua nyingine, alisema pamoja na serikali kufanya kazi nzuri kusaidia wanawake,bado kuna urasimu wa sera na mifumo isiyo rafiki kwa wajasiriamali wadogo.

Akizungumza Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi,Danford Kamenya, alisema katika kipindi cha mwaka 2016/17 Manispaa hiyo imetoa Sh.234milioni,kwa vikundi vya wanawake 53,ikiwa ni hatua mojawapo ya kuwawezesha kiuchumi.

Alisema katika kupindi cha mwaka 2017/2018, imetolewa Sh. 195Milion, kwa vikundi 39 na kwamba fedha hizo zimewawezesha wanawake kuanzisha shughuli za ujasiriamali na kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake Naibu Meya wa Manispaa ya Moshi  Mh.Peter Minja,alisema soko limekuwa tatizo kwa wajasiriamali wengi na kushauri wajasiriamali kutengeneza bidhaa zenye ubora ili kuweza kuingia kwenye ushindani.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi