• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MH.JAFO AITAKA MANISPAA KUHARAKISHA UJENZI WA KITUO CHA MABASI NGANGAMFUMUNI

Posted on: December 22nd, 2018

Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Seleman Jafo amefanya ziara katika kituo kikuu cha mabasi kilichopo Manispaa ya Moshi na kusisitiza kuanza haraka kwa wakati ujenzi wa kituo kipya cha mabasi cha Ngangamfumuni kitakachogarimu tsh bilioni 27.

Akiwa katika kituo kikuu cha Mabasi Waziri Jafo alisema Manispaa  imefikia katika  hatua nzuri kwa kumpata mkandarasi wa ujenzi,ambapo tayari Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni saba kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha kisasa cha mabasi.

Waziri Jafo pia aliitaka Manispaa ya Moshi kuharakisha mchakato wa kuanza kwa ujenzi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha malengo ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa mradi huu yanafikiwa na endapo Manispaa  itaendelea kuchelewa kutumia fedha hizo  Serikali  haitasita kuzihamishia fedha hizo kwenye Halmashauri nyingine.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi, Raymond Mboya, alisema miongoni mwa mambo yanayoweza kusababisha kuchelewa kuanza kwa ujenzi wa kituo cha Ngangamfumuni ni pamoja na kusubiriwa kwa kibali kutoka hazina.

“Tayari Serikali imekwishatoa kiasi cha tsh bilioni 7 lakini tunajua kuwa ujenzi wa kituo hiki utagharimu zaidi ya bilioni saba tunakuomba utusaidie kusukuma ili tuweze kupata kibali toka hazina kitachotuwezesheza kukopa fedha kutoka benki ya TIB ili ujenzi wa kituo uweze kukamilika kwa wakati”Alisema  Mboya.

Akitoa taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa kituo kipya cha mabasi cha Ngangamfumuni Mkurugenzi wa Manispaa  Michael Mwandezi alisema kuwa tayari tumekwishampata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha hicho na tunatarajia ujenzi utaanza rasmi mwenzi Januari mwaka 2019.

“Mh Waziri tunakuhakikishia kila kitu kinaenda vizuri na mchakato wa kumpata mkandarasi ulizingatia taratibu zote za manunuzi ikiwa ni pamoja na kushirikisha viongozi ngazi ya Mkoa ambapo mwezi Januari tutasaini mkataba na  mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi”Alisema Mwandezi.

Baadhi ya wadau wa usafirishaji wameeleza kuwa kujengwa kwa kituo kipya cha mabasi kutapunguza kero ya msongamano iliyopo katika  kituo kikuu cha mabasi kinachotumika kwa sasa hivyo kuomba Serikali kuharakisha ujenzi wake.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi