• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MBUNGE WA MHE PRISCUS TARIMO AMEIPONGEZA MANISPAA KWA USIMAMIZI WA MIRADI

Posted on: July 11th, 2024


Mbunge Moshi Mjini Mhe. Priscus Tarimo amempongeza Mkurugenzi na Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa Manispaa.

Amesema kwa kipindi cha Miaka 3 ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan serikali imetoa fedha za miradi ya Maendeleeo zaidi Sh. Billioni 23 ambazo zimetumika katika ujenzi wa Shule Mpya, Madarasa, Jengo la Utawala, Vituo vya afya na hospitali ya Manispaa.

Tarimo ameyasema hayo leo, Julai 11, 2024 wakati wa uzinduzi wa Madarasa 9 shule ya Sekondari Mawenzi ambao utekelezaji wake umegharimu zaidi ya Sh,234 milioni.

Mbunge Tarimo alitembelea na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa ndani ya Manispaa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hospitali ya Manispaa, bweni la wavulana shule ya Sekondari Msandaka, shule ya Sekondari Lucy Lameck, Ukarabati wa shule ya msingi Mwenge, ujenzi wa jengo la utawala la Manispaa hiyo ambalo limegharimu zaidi ya Sh2 bilioni.

"Leo tulikuwa tunakagua miradi ambayo inatekelezwa na serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, miradi hii imejengwa kwa ubora na kwa kiwango kinachotakiwa,"

Amelipongeza baraza la Madiwani, Mkurugenzi na Menejimenti ya Manispaa kwa kusimamia vizuri na kwa ubora ujenzi wa miradi hiyo na kwamba ameridishwa nayo kutokana na kasi ya ujenzi huyo ambao amesema serikali imeleta fedha kwa ajili ya kuhakikisha kipaumbele cha elimu pamoja na mambo mengine inazingatiwa.

"Tumetembelea mradi wa ujenzi wa hospitali yetu ya Wilaya nimeridhishwa na ujenzi unaoendelea inatekelezwa vizuri sana, pia tumetembelea shule za Sekondari ambazo zimejengwa awamu hii, tumetembelea shule ya Sekondari Lucy Lameck, shule ya Sekondari Msandaka ambapo tumekamilisha ujenzi wa bweni la wavulana,"

Pamoja na mambo mengine ameishukuru serikali kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa shule kongwe zilizopo katika Manispaa hiyo ambazo zilijengwa miaka 50 iliyopita.

"Naleta salamu za upendo za Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupokea mipango yote tuliyopeleka kwa ajili ya Jimbo la Moshi mjini na imetejekezwa,"amesema Mbunge huyo

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Sekondari Mawenzi, Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Moshi, Agness Luwhavi amesema serikali imetoa zaidi ya Sh234 milioni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 9 katika shule ya Sekondari Mawenzi ambayo ujenzi wake umekamilika.

Amesema ujenzi wa madarasa haya ni moja ya nia ya Serikali ya kuhakikisha inaboresha miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi.

"Tunaishukuru serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizi za vyumba 9 vya madarasa kwa manufaa ya kikazi cha Sasa na cha baadaye,"amesema

Naye, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Mwajuma Nasombe ameishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo kwenye miradi ya shule, hospitali pamoja na barabara.


"Tunaishukuru serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha nyingi za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Manispaa yetu,"amesema Nasombe

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi