• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MANISPAA YA MOSHI YAZINDUA MAGARI MAPYA MATATU YA UZOAJI TAKA

Posted on: December 20th, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imezindua magari mapya matatu ya uzoaji taka ikiwa ni juhudi za kumuunga Mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Joseph Magufuli za kuhakikisha Mji wa Moshi unaendelea kufanya vizuri katika nyanja ya usafi na utunzaji wa mazingira.

Uzinduzi wa magari hayo mapya umefanywa na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba katika viwanja vya ofisi za manispaa Moshi na kuifanya  Manispaa kuwa na idadi ya magari nane ya kisasa  kwa ajili ya uzoaji wa taka ngumu.

Akizundua magari hayo Kippi Warioba alisema kuwa Manispaa ya Moshi imekuwa ikifanya vizuri kwa muda mrefu kwenye suala la usafi na utunzaji wa Mazingira hivyo ujio wa magari hayo utaifanya iendelee kufanya vizuri zaidi huku washindani wake wakiwa ni Manispaa na Majiji na siyo Halmashauri .

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Michael Mwandezi, magari hayo matatu ambayo ni compactor mbili(magari ya kushindilia taka)  na skip master moja (gari la kubeba maghuba ya taka) yote kwa pamoja yana thamani ya ths. milioni 613, 522,000 ambayo yataamaliza tatizo la uzoaji taka kwa kuzoa taka tani 96 kwa siku.

Alisema kuwa halmashauri ilikuwa na magari matano ambayo yalikuwa na uwezo wa kuchukua kiasi cha tani 156 za taka kwa siku ambapo kwa Manispaa ya Moshi yenye wakazi takribani 206,728  inazalisha taka tani 238 kwa siku.Baada ya kuongeza magari haya ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kubeba na kushindilia taka manispaa ya Moshi itakuwa na uwezo wa kuchukua taka zote zinazozalishwa kwa siku.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi alisema Manispaa Raymond Mbowe alisema Manispaa ya Moshi  ipo kwenye mchakato wa ujenzi wa dampo la kisasa pamoja na  kujenga kiwanda kitachotengeneza  mbolea  kwa kutumia takataka ambacho kitatoa fursa ajira kwa wananchi na kugeuza takataka kuwa mali.

Alisema lengo la Manispaa ya Moshi ni kuendelea kuwa kinara wa katika usafi na utunzaji wa Mazingira hapa nchini hivyo watahakikisha wanayatunza magari  mapya pamoja na kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya matengenezo ya  magari ya uzoaji taka  ili kuweza kutekeleza vyema suala la usafi wa mazingira.

“Pamoja na kununua magari  haya matatu Manispaa ya Moshi imeanza mchakato wa kununua gari lingine la kisasa kwa ajili ya uzoaji wa taka kwa fedha zilizotengwa kwenye bajeti ya mwaka 2018/2019”Alisema

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi