• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MANISPAA YA MOSHI YAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA USAFI

Posted on: September 10th, 2022

HALMASHAURI ya Manispaa ya Moshi imeanza mikakati ya kuimarisha usafi wa mazingira kwa kuhakikisha utekelezwaji wa sheria ndogo ya usafi na Mazingira ya mwaka 2006 na Marekebisho yake ya mwaka 2019 inafuatwa ili kuendeleza sifa ya Manispaa ya  Moshi ya kuwa Manispaa safi ikilinganishwa na Manispaa nyingine hapa nchini.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Ndg. Rashid Gembe ambapo amesema ili kufikia azma hiyo, uongozi wa Halmashauri   utahakikisha sheria hii inatekelezwa vilivyo na ukamataji wa wachafuzi na waharibifu  wa mazingira watakamatwa na kutozwa faini ya papo kwa papo isiyopungua kiasi cha Shilingi Elfu Hamsini au kifungo cha miezi sita jela.

“Sheria hii inapiga marufuku utupaji wa taka ovyo, utemaji wa makohozi, utiririshaji wa maji ovyo pamoja na kujisaidia ovyo ambapo kwa yeyote atakayetenda makosa hayo atatozwa faini ya papo kwa hapo isiyopungua Shilingi Elfu Hamsini” Alisema Gembe

Mikakakati mingine iliyowekwa ni pamoja na kuboresha mbao za  matangazo ili kuelimisha jamii kuhusu usafi na utunzaji wa Mazingira sehemu mbalimbali za mji, kutoa matangazo kwa vipaza sauti kwenye masoko na kituo kikuuu cha mabasi, kupitisha gari la matangazo na kuendelea kushirikiana na vyombo vya Habari ili kuwakumbusha wakazi wa Manispaa ya Moshi wajibu wao juu ya usafi na utunzaji wa Mazingira.

Aidha alisema mikakati hiyo itahusisha pia ukusanyaji wa taka za aina mbalimbali zinazozalishwa katika mitaa yote ndani ya Manispaa na sehemu ya taka hizo zitatumika  kwa ajili ya uzalishaji wa mbolea kwenye Kiwanda cha mbolea cha mboji kilichoko eneo la Mtakuja kinachomilikiwa na kuendeshwa na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa kushirikiana na Mji rafiki wa Tubingen uliopo chini Ujerumani.

“Hadi kufikia mwezi Agosti, mwaka huu, takwimu zinaonesha kuwa mji wa Moshi unazalisha jumla ya tani 236 za taka  kila siku yakiwemo mabaki ya mboga mboga na matunda ambayo ni mali ghafi ya Kiwanda cha mboji na uzalishaji huo ni sehemu ya kuufanya mji wetu uwe safi”, alisema.

Gembe alisema nia ya mpango huo kabambe ni kuhakikisha Manispaa ya Moshi inandelea kushika nafasi yake ya kwanza katika Mashindano ya Usafi wa Mazingira yanayofanyika kila mwaka kwa uratibu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii.

“Ushindi wetu wa kila mwaka kwa miaka mingi mfululizo ulikuwa chachu ya miji mingine hapa nchini kuiga mfano wetu katika kuhakikisha mji unakuwa safi ambapo Halmashauri nyingi zimefanya ziara za mafunzo kuja kujifunza  jinsi tulivyofanikiwa kufanya mji wetu kuwa safi na kuwa kinara wa usafi hapa nchini”, alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi