• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MANISPAA YA MOSHI YASAINI MAKUBALIANO YA KUSHIRIKIANA NA JIJI LA MARBURG-UJERUMAN

Posted on: October 26th, 2023

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na Jiji la Marburg Ujerumani zimesaini Makubaliano ya Kiungwana kwa ajili ya ushirikiano katika Sekta ya Afya, Michezo na Nyanja mbalimbali zinazohusiana na masuala ya maendeleo ya jamii.

Makubaliano hayo yamesainiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo na Mstahiki Meya wa Jiji la Marburg Dkt. Thomas Spies, katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa Moshi, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo alisema ushirikiano wa Miji hii Miwili vile vile utahusisha ushirikiano katika sekta za Majanga na Zimamoto.

“Marburg ni Jiji ambalo limejikita kwenye masuala ya elimu zaidi hususani ile inayohusiana na afya tib ana kinga  hivyo ushirikiano huu utakuwa ni muhimu sana katika kuboresha sekta ya afya katika Manispaa yetu”, alisema.

Aidha alisema Jiji la Marburg pia limebobea katika  kupambana na Majanga eneo la uokoaji hasa Zimamoto hivyo uhusiano huu utasaidia kupata vifaa vya Zimamoto Pamoja na Elimu juu ya uokoaji na kupamabana na Majanga kama vile mafuriko na matetemeko ya ardhi.

“Ujumbe wa Mstahiki Meya wa Marburg na ujumbe wake watatembelea kituo chetu cha zimamoto, maeneo ya kutolea huduma za afya yaliyo chini ya Halmashauri ya Manispaa Moshi, ili kujionea shughuli zinazofanyika ili kuweza kupata mwanga wa jinsi ya  utekelezaji wa ushirikiano wetu mpya tulioingia rasmi leo tarehe 25/10/2023 ”, alisema.

Mstahiki Meya Kidumo pia alisema ujumbe huo utatembelea miradi ya michezo inayotekelezwa Manispaa ya Moshi ikiwemo ukarabati wa uwanja wa michezo wa Majengo pamoja na vituo vya kukuzia vipaji vya michezo.

“Katia ujumbe huu pia kuna Mtaalamu wa michezo ambaye tayari ameoneysha nia ya kusaidia kukuza vipaji vipya kwa kutoa ufadhili na msaada wa kiufundi katika vituo vya kukuza vipaji Manispaa ya Moshi”, alisema.

Vile vile Mstahiki Meya alisema ndani ya makubaliano hayo tunategemea watumishi wa Jeshi letu la Zimamoto wanatakuwa wanapata  mafunzo ili kuboresha hali ya uokoaji na kupambana na majanga mbalimbali yanapotokea.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Marburg Dkt. Spies alielezea kufurahishwa kwake na kuanzisha Uhusiano huu  mapya kati ya Miji hii Miwili na kuongeza kuwa Uhusiono huu unalenga kuboresha maisha ya  wananchi  wa pande zote mbili.

“Kwa miaka mingi wananchi wa Marburg wanaamini katika ushirikiano na Halmashauri za Manispaa na Majiji mengine na Moshi ni eneo lao la saba katika kuanzisha ushirikiano wa aina hii”, alisema Dkt. Spies

Alisema wazo la kuunda ushirikiano kati ya Manispaa ya Moshi na Jiji la Marburg ni katika kubadilishana mawazo, kushirikiana katika kutambua na kufuatilia tamaduni za pande zote mbili na pia kila upande kupata fursa ya kujifunza utamaduni ya upande mwingine.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi