• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MANISPAA YA MOSHI YAFANIKIWA KUTOA MIKOPO YA ZAIDI BIL 1.8 KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO

Posted on: October 23rd, 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi Tsh Bilioni 1.8 kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kwa kipindi cha miaka mitano 2015-2020 ya utawala wa Rais wa awamu ya 5 Dr. John Joseph Magufuli  kwa lengo la kuinua kipato cha wananchi.

Hayo   yamebainishwa na Mkuu wa Idara  Maendeleo ya jamii Manispaa ya Moshi, Rose Njau  wakati wa utoaji wa mikopo kwa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ambapo Halmashauri imetoa mikopo yenye thamani ya Tsh milioni 281 kwa vikundi vya wanawake na Vijana.

“Kumekuwepo na mwitikio mkubwa kwa makundi yote ukiacha kundi moja la watu wenye ulemavu,ambapo tumekuwa tukisisitiza kujikita katika kuanzisha miradi yenye tija ili kuweza kupata matokeo chanya kwenye uchumi wa wananchi na taifa”Alisema Rose Minja

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwanasheria  wa Manispaa ya Moshi Iddi Ndabhona alisema  mafanikio makubwa yameonekana kutokana na mikopo isiyokuwa na riba kwa vikundi wajasiriamali  hivyo kwasasa wajasiriamali wanapaswa kujikita kuanzisha viwanda vidogo ili kuleta matokeo chanya kwenye uchumi wa viwanda.

“Leo tumetoa mkopo kwa vikundi vya wanawake 30 wenye thamani ya Tsh Milioni 172,vikundi 12 vya vijana milioni Tsh. 109, ambapo kwa awamu hii hatujafanikiwa kupata maombi ya vikundi vya watu wenyeulemavu hivyo Halmashauri inaendelea kuhamasisha na kusisitiza walemavu wajitokeze kwa ajili ya kupata mikopo hii isiyokuwa na riba”Alisema. Idd Ndabhona

Nao wanavikundi wanaeleza kuwa mikopo inayotolewa na Halmashauri ambayo haina riba imekuwa na mchango mkubwa kwenye miradi yao, pamoja na kukuza kipato cha mwananchi mmoja mmoja na kuchangia pato la taifa.

Kwa mujibu wa sheria ya usimamizi na utoaji wa mikopo ya mwaka 2019 halmshauri zote nchini zinapaswa  kutenga asilimia 10 ya mapato yake ili kuwezesha vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi