• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MANISPAA YA MOSHI YA SAINI MAKUBALIANO YA KUSHIRIKIANA NA JIJI LA SUNCHEON KOREA YA KUSINI

Posted on: May 21st, 2018


UJUMBE wa watu watano kutoka mji wa Suncheon nchini Korea Kusini ukiongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji hilo Mr.Choong-Hoon Cho wametembelea manispaa ya Moshi na kusaini makubaliano ya kiungwana na Halmshauri ya Manispaa ya Moshi  kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo katika masuala ya Sayansi na Teknolojia.Mbali na hilo pia wamekubaliana kushirikiana na kubadililishanauzoefu katika sekta ya Elimu,utamaduni pamoja na kubadilishana wa jinsi ya kutunza taka ngumu na utunzaji wa Mazingira.


Akizungumza Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Michael Mwandezi alisema kuwa, ujio wa Meya huyo wa korea na wajumbe wake unatokana na juhudi za serikali kuboresha mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na mataifa mbalimbali Duniani.


"Kama unavyojua, serikali ya Tanzania imefungua Ubalozi wakeKorea ya Kusini  mwaka huu, na hii imefungua milango ya kibiashara katika nchi hizi mbili na ndio maana umeona Mstahiki Meya wa jiji Suncheon Korea amekuja na wajumbe wake kutembelea Manispaa yetu ya Moshi, hii ni fursa kubwa sana ya kutangaza bidhaa zetu na fursa za uwekezaji zilizopo Manispaa ya Moshi ..." alisema Mwandezi.


Naye  Mstahiki Meya wa mji wa Suncheon nchini Korea Kusini,Choong-Hoon Cho,   alitoa wito kwa serikali yaTanzania kuitangaza vyema kahawa ya Kilimanjaro kwa kuwa ina ladha ya kipekee kuliko kahawa nyingine yeyote inayolimwa Duniani.


“Kahawa ya Kilimanjaro inaonekana kuwa na ladha ya kipekee tofauti na Kahawa ambayo inatoka nchi nyingine; kwani tulipofika katika Mkoa wa Kilimanjaro hususani katika Manispaa hii tumekunywa kahawa hakika ni tofauti na nzuri kuliko ambayo tunaletewa na kunywa huko kwetu”Aliongeza“Tutakwenda kuwashawishi wafanyabiashara wa Korea ya Kusini kuja Manispaa ya Moshi kuwekeza na kuchukua kahawa ya Tanzania na kuipeleka Korea,ninatoa wito kwa serikali ya Tanzania kuhakikisha inatangaza za bidhaa zao zaidi ili ziweze kujulikana kimataifa kwani inaonekana kuna bidhaa bora lakini hazijulikani hasa kwenye nchi kama niliyotoka mimi.” anafafanua Meya huyo.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi Raymond Mboya alifafanua kuwa Manispaa ya Moshi na Mji wa Suncheon wamekubalina kushirikiana katika mambo mbalimbali ikiwemo kwenye sekta ya Elimu, utamaduni, Uchumi, Mazingira pamoja na michezo.

Aidha alielezea kuwa katika ziara hii,ugeni huu umetembelea shule ya sekondari ya ufundi ya Moshi, shule Msingi ya Mwereni , shule ya Mother Theresa Daycare Centre, Chuo Kikuu cha Ushirika, Hifadhi ya mlima Kilimanjaro Kinapa na hifadhi ya taifa ya Manyara.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi