• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

Posted on: January 27th, 2025

SERIKALI ya awamu ya sita imetoa jumla ya shilingi bilioni 956.63 kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo tangu Rais Dk Samia Suluhu Hassan aingie madarakani mwaka wa 2021.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw Nurdin Babu wakati wa hafla maalum ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais Dk Samia iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Majengo ulioko Manispaa ya Moshi, mkoani humo, Jumatatu.

“Kiasi hili ni kikubwa ikilinganishwa na jumla ya shilingi milioni 285 ambazo zilishatolewa kwa kipindi cha miaka 25 iliyopita; hii ni hatua kubwa kwa ajili ya maendeleo ya Mkoa wa Kilimanjaro”, alisema.

Bw Babu alisema kuwa kupitia fedha hizo tayari miradi 1,360 imetekelezwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo kwenye sekta za afya, elimu na miundombinu mbalimbali ikiwemo ya maji na barabara.

“Katika fedha hizo, jumla ya 117.08 bn/- zimetumika kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa taasisi za kiafya 289, pamoja na ununuzi wa dawa na vifaa tiba”, alisema na kuongeza, manispaa ya Moshi, imepokea jumla ya 3bn/- kwa ajili ha ujenzi wa hospitali ya wilaya ambayo alisema itakuwa ni ya ghorofa.

Aliendelea kusema kuwa katika sekta ya elimu Mkoa ulipokea jumla ya 149.64bn/- ambazo alisema zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mapya 1,82, shule mpya 44 zikiwemo za msingi na sekondari, ujenzi wa mabweni 106, matundu ya vyoo 305, maabara 181, shule shikizi 5, vuo vya kati pamoja va vyuo vikuu.

Aidha alisema Serikali pia imetenga fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya utalii ambayo yamechangia kuongezeka kwa watalii wanaoingia hapa nchini ikiwemo kupanda Mlima Kilimanajro ambao ndiyo mrefu kuliko yote Barani Afrika.

Bw Babu alisema kuwa kutokana na Rais Dk Samia kuwa kinara katika kuboresha na kulinda mazingira nchini, shughuli za sherehe ya kuzaliwa kwake zimeanza kwa viongozi mbalimbali wa ngazi za wilaya na Mkoa kupanda miti katika shule ya sekondari ya Lucy Lameck, iliyoko manispaa ya Moshi.

Katika hafla hiyo mbali na shughuli za kupanda mti, pia Bw Babu alikata keki maalum kwa ajili ya kuadhimisha sherehe ya kuzaliwa kwa Rais Dk Samia, ikiwa ni moja wapo ya keki zilioandaliwa kwenye hafla hiyo ambazo ziligawiwa kwa waliohudhuia hafla hiyo.



Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi