• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Madiwani wapewa Mafunzo ya Sheria Ndogo na Maadili ya Utumishi wa Umma

Posted on: February 6th, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, imetoa mafunzo ya sheria ndogondogo na maadili kwa Madiwani, lengo likiwa ni kukumbushana masuala ya maadili  na  kuimarisha ushirikiano kati ya madiwani na watendaji ili kuboresha ukusanyaji wa mapato ya ndani.


Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna

Mghwira, alisema Mafunzo haya yatakuwa chachu kwa Madiwani na kuboresha ushirikiano kati ya madiwani na watendaji kwa nia ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Manispaa ya Moshi.


Alisema lengo la Msingi la mafunzo hayo ni kuwawezesha Madiwani,

kupata uelewa wa sheria ndogondogo za ukusanyaji wa ada na ushuru

mbalimbali kwa ajili ya kuiwezesha Halmashauri, kupata mapato ambayo

yatafanikisha na kurahisisha utekelezaji wa shughuli za utoaji huduma

bora kwa wananchi.


Mghwira alisema Ushirikiano katika utumishi wa Umma unajengwa katika

msingi wa mgawanyo wa majukumu ya kiutumishi, na kuwataka madiwani

kutumia mafunzo hayo  kuibua ushirikiano mpya katika

utendaji kazi wakishirikiana  na watendaji wa Halmashauri .


"Waheshimiwa Madiwani, ninyi ni watumishi wa umma kwa kuwa mnashika

nafasi ambazo mnawatumikia wananchi,hivyo mafunzo haya ya sheria

ndogondogo  za ada na ushuru mbalimbali pamoja na maadili,yawezeshe

kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja kati yenu na watendaji,katika suala

zima la ukusanyaji wa mapato ndani ya Halmashauri"alisema Mghwira.


Mkuu wa Mkoa alitumia pia nafasi hiyo kuwataka madiwani kutumia

mafunzo hayo, kufanikisha shughuli za ukusanyaji wa

mapato,utayarishaji wa taarifa fasaha,sahihi na za kuaminika, ambazo

zitatumika kama rejea katika kuamua mwelekeo wa Halmashauri katika

suala zima la Mapato.


Akizungumza Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,

Bwana Michael Mwandezi, alisema  watazingatia mada zote

zitakazofundishwa kwani zitasaidia kuiwezesha Halmashauri yake  kukusanya

mapato yaliyokusudiwa.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti  baadhi ya madiwani walioshiriki mafunzo hayo,walisema mafunzo watakayoyapata yatakuwa chachu ya kuwawezesha kusimamia na

kutekeleza sheria ndogondogo za ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, pamoja na kuzingatia  maadili ya utumishi wa Umma.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi