• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

HALMASHAURI ZAJIFUNZA SIRI YA MAFANIKIO YA USAFI

Posted on: March 26th, 2018

Mafanikio ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, kushawishi wananchi wake kuchangia ada ya taka kwa ajili ya ukusanyaji na uzoaji taka katika ngazi ya kata ‘umeziduwaza’ halmashauri za Jiji la Mwanza, Manispaa ya Ilemela na Manispaa ya  Morogoro.

Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira wa Jiji la Mwanza, Viane Kombe alisema mafanikio hayo ya Moshi, ndiyo yaliyowasukuma maafisa afya na watendaji wa kata katika halmashauri hizo tatu kutembelea Manispaa ya Moshi kujifunza masuala ya  usafi na utunzaji wa Mazingira pamoja na jinsi ya kugeuza taka kuwa mali.

“Kuja kwetu Moshi ni kutaka kujifunza wenzetu wanafanyaje usafi, siri ya mafanikio yao na gharama halisi za kuendesha zoezi la ukusanyaji taka mitaani, wao wametwaa mara nyingi tuzo za mashindano ya taifa ya afya na usafi wa mazingira inayohusisha halmashauri za majiji, manispaa, miji na wilaya 73 nchini,”alisema

Manispaa ya Moshi iliendelea kuongoza  halmashauri majiji na manispaa baada ya kuwa mshindi wa kwanza kitaifa mwaka jana  kwa kupata asilimia 78.5, ikifuatiwa na Jiji la Arusha iliyopata asilimia 78.1 na Manispaa ya Iringa asilimia 67.2

Akitoa siri ya mafanikio hayo, Afisa Mtendaji wa Kata ya Mawenzi, Erasmo Silayo alisema eneo lake ambalo lina kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na ambalo ndio kitovu cha mji huo limejiwekea utaratibu mzuri wa ukusanyaji fedha za usafi, ambapo kwa mwaka mmoja hukusanya kiasi cha Sh. milioni 45 kama ada.

Fedha hizo hutumika kulipa vibarua 17 wanaofanya kazi ya kufagia mitaani na wale wanaotembea na magari ya taka, kununua mafuta ya gari linalohudumia kata hiyo mara tatu kwa wiki.Wananchi humasishwa kuhifadhi takataka katika vyombo vya kuhifadhia taka ngumu na huzitoa taka hizo wakati ambapo gari linapopita.

“Wananchi wetu wamejengewa utaratibu wa kuchangia ada ya uzoaji taka, tumekuwa tukitoa demand notes (hati ya madai) kila mwanzo wa mwaka wa fedha, kwa biashara zote na ngazi ya kaya, tuna viwango tofauti, kwa mfano kwa wafanyabiashara tunaanzia 780,000 mpaka 36,000 ambayo ni kiwango kidogo kabisa. Katika ngazi ya kaya tunachukua shilingi 12,000 kwa mwaka kwa maana ya kwamba kila mwezi kaya inachangia shilingi 1, 000”alifafanua Silayo

Aidha, Kaimu Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira wa Manispaa ya Moshi, Bernadeta Mtei alisisitiza pamoja na mafanikio hayo, Manispaa hiyo kwa siku moja inazalisha kiasi cha tani 256 za taka na kwamba kwa wale wachache ambao  ni wakaidi kuchangia ada ya taka  hufuatiliwa na uongozi wa kata na kuadhibiwa kwa mujibu wa  sheria ndogo ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ya Mwaka 2006 pamoja na Marekebisho yake.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi