• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

FEDHA ZA TOZO ZAENDELEA KUBORESHA SEKTA YA AFYA MANISPAA YA MOSHI

Posted on: September 15th, 2022

SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha sekta ya afya kupitia fedha za tozo ambapo safari hii jumla ya shilingi milioni 250 zilizotolewa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi zinatarajiwa kutumika katika kuboresha kituo cha afya cha Shirimatunda kilichopo Kata ya Shirimatunda.

Mkurugenzi wa Manispaa Ndg. Rashid Gembe amesema fedha hizi zitatumika katika upanuzi wa kituo hicho kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya Mama na Mtoto, jengo la upasuaji, njia ya kupitia wakati wa kutoa na kupata huduma (walkway) na jengo la kufulia.

“Moboresho haya yatasaidie kutoa huduma kwa karibu zaidi kwa wagonjwa ambao walikuwa wakisafiri mwendo mrefu kutoka kata ya Shirimatunda na Kata za jirani kwenda hospitali ya rufaa ya Mkoa au ile ya rufaa ya Kanda ya KCMC kufuata huduma ambazo zitapatikana baada ya maboresho ya kituo hiki”, alisema.

Gembe aliendelea kusema kuwa mbali na wakazi wa kata ya Shirimatunda, Soweto na  Karanga kunufaika na maboresho hayo pia wananchi walioko maeneo ya vijiji vya Shirimgungani na Mijengweni wilaya ya Hai watanufaika na maboresho hayo.

Kwa mujibu wa Gembe hiyo ni awamu ya pili ya fedha kutolewa na Serikali kwa ajili ya maboresho ya kituo hicho cha Shirimatunda kufuatia jumla ya shilingi milioni 250 zilizotolewa awali ambazo alisema zilifanikisha ujenzi wa jengo la kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) na maabara katika kituo hicho jambo ambalo alisema limewaongezea ari ya kufanya kazi wahudumu walioko kituoni hapo.

“Mbali na watumishi kuridhika, maboresho haya pia yamewahamasisha wananchi na kusababisha idadi ya watu wanaopata huduma katika kituo hicho kuongeza kutoka wastani wa watu 20 na 25 kwa siku na kufikia 30 na 35 kwa siku”, alisema.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mhandisi Zuberi Kidumo ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo za Tozo ambapo amesema kuboreshwa kwa huduma katika kituo hichi ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025 lengo lake ni kutoa huduma bora na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.

“Nichukue fursa hii kwa niaba ya wananchi wa Manispaa ya Moshi kuipogeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ilivyokuwa mstari wa mbele katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi na jinsi ilivyokuwa mstari wa mbele kuboresha huduma za afya na kusogeza huduma hizo kwa wananchi.”, alisema.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi