• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Baraza la Madiwani lakasirishwa na Harufu Mbaya ya Kiwanda Cha Ngozi

Posted on: February 2nd, 2018

BARAZA la madiwani la Halmashauri ya manispaa ya Moshi,  limeazimia kuandika barua kwa  Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa  Mazingira (NEMC) kushawishi kukifunga kiwanda cha ngozi cha Moshi kwa madai ya kukiuka sheria za mazingira na kuathiri afya za wananchi.


Kiwanda hicho kilichopo katika kata ya Njoro, kimekuwa kikilalamikiwa kwa muda mrefu na wananchi kutokana na kutoa harufu mbaya inayosambaa katika makazi yao hali ambayo imekuwa ikiathiri afya zao .


Akitoa  azimio hilo kwa niaba ya wajumbe wa  baraza , Naibu mstahiki meya  Peter Minja, alisema kiwanda hicho kimegeuka kero kwa wananchi kutokana na kukiuka sheria za mazingira kwa muda mrefu hali ambayo imekuwa ikihatarisha afya za wakazi wa  eneo hilo.

Alisema licha ya halmashauri  kufanya jitihada za kuhakikisha mwekezaji wa kiwanda hicho anafuata taratibu, na sheria za mazingira ikiwemo kuthibiti harufu hiyo ambayo imekuwa kero kwa wananchi, amekuwa kitoa ahadi ambazo hazitekelezi .

“Mkurugenzi tunakuagiza uandike barua NEMC ueleze namna harufu hii inavyo waathiri wananchi afya zao.”alisema

Aliendelea kusema kuwa “Barua hii iandikwe haraka iweezekanavyo  na  isiishie hapo tu… menejimenti tunaomba muende pale kiwandani mfanye ukaguzi kwani muwakilishi wa kiwanda katueleza  kuwa kunamashine wamefunga tayari za kutibu maji taka  na kuzuia hiyo harufu mjiridhishe kama kweli zoezi hilo limefanyika”alisema.

Akizungumza  kabla ya kupitishwa kwa azimio hilo Diwani wa kata ya Bomambuzi  Juma Rahibu, alisema kiwanda hicho kwa miaka mingi kimegeuka kero kwa wananchi wanaoishi katika kata hiyo na kata nyingine za pembezoni jambo ambalo halipaswi kufumbiwa macho na  mamlaka zinazo husika.

Naye Diwani wa kata ya Rau ,Peter Kimaro alisema kiwanda hicho kimekuwa kikitoa matumaini kwa halmshauri hiyo kwamba wanauwezo wa kudhibiti harufu hiyo tangu mwaka 2013 na kwamba sasa ni miaka mitano imepita na suala hilo bado halijatafutiwa ufumbuzi hivyo ni vema hatua za kisheria  zifuatwe ili kunusuru afya za wananchi.

 “Kiwanda hichi kilishapigwa faini ya shilingi milioni 32 na NEMC yenyewe kutokana na kukiuka sheria za mazingira lakini pamoja na faini hiyo bado  hawajafanya marekebisho  yoyote  hivyo tuwajulishe ili waone ni taratibu gani za kisheria zinapaswa kufuatwa kwa sasa”alisema Priscus Tarimo Diwani wa Kata Kilimanjaro

Danford Kamenya, kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, alisema watafika kiwandani hapo kufanya ukaguzi ili kuona  kama mashine za kudhibiti harufu zimefungwa, kama ilivyokuwa makubaliano ya awali.

“Kiwanda hiki tulikiagiza kifunge mashine za kudhibiti harufu, na zoezi hilo lilitakiwa kukamilika April 2017, lakini walidai kazi hiyo ni kubwa itahitaji muda, na wamekamilisha Disemba 2017, sasa tutakwenda kuwakagua kama wametekeleza hilo na tukikuta hawajafanya, tutaandika barua NEMC ili wao waone ni hatua zipi za kisheria watachukua”alisema Kamenya.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA MANISPAA YA MOSHI April 17, 2025
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI

    April 10, 2025
  • BAJETI YA KIMKAKATI WA KUONGEZA MAPATO YA NDANI

    February 07, 2025
  • MAMA SAMIA ATOA TSH. BILLIONI 956 KWA AJILI MIRADI YA MAENDELEOA MKOA WA KILIMANJARO

    January 27, 2025
  • MANISPAA YATOA MIKIPO ISIYO NA RIBA ZAIDI YA TSH. BILLION 1.1

    January 20, 2025
  • Tazama

video

ZAWADI YA USAFI YARUDI NYUMBANI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi