• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Moshi Municipal Council
Moshi Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • History
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhamira
      • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
        • Elimu ya awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mipango Takwiku na Ufuatiliaji
      • Afya Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Elimu ya awali na Msingi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Teknolojia Habari Mawasiliano na Uhusiano
      • Ununuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Election
    • Muundo wa Kiutawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Michezo na Utamaduni
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango Miji
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

leseni

HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOSHI 

 

UTARATIBU WA KUPATA LESENI ZA BIASHARA

 

 

  • UTANGULIZI

 

Leseni ni kibali halali kinachotolewa na mamlaka husika kwa ajili ya kufanya biashara

iliyoombwa kulingana na aina ya biashara ikionyesha eneo linalopaswa kufanyika biashara kwa

mujibu wa Sheria.

AINA YA LESENI ZA BIASHARA

 

Zipo aina mbili (2) kuu za leseni.

1. Leseni za biashara zinazosimamiwa na sheria No. 25 ya mwaka 1972 na marekebisho

yake mwaka 2004. Mfano : Leseni za Hoteli, Maduka ya rejareja n.k

2. Leseni za vileo zinazosimamiwa na sheria No 28 ya mwaka 1968 na marekebisho yake

ya 1990.

(C) ILI MFANYABIASHARA APATE LESENI YAFUATAYO NI LAZIMA

YATEKELEZWE ( Kwa kundi la 1)

 

1. Kila mfanyabishara anatakiwa kuomba leseni kwa kujaza fomu za maombi ya leseni

zinazotolewa na Halmashauri kupitia kitengo cha Biashara kwa gharama ya Tshs. 1000/=

tu

2. Kila mfanyabiashara lazima awe na kibali cha kodi ya mapato (Business Tax Clearance

Certificate (BTCC) na Tax Identification Number (TIN).

3. Kwa biashara zilizosajiliwa Brela mfanyabishara ataambatanisha vyeti vya usajili yaani

Certificate of Registration, Extract from Register na Cerificate of Incorporation (Kwa

Makampuni) Pamoja na Hati ya Makubaliano (Memorundum and Articles of

Association).

(D)WAOMBAJI WAPYA:

Mfanyabiashara atatakiwa kujaza fomu ya maombi na kupitisha sehemu zifuatazo:

 Kupitisha kwa Afisa Mtendaji wa Kata husika.

 Kupitisha kwa Afisa Ardhi/Mipango Miji (kwa baadhi ya Biashara

Mfano: Uoshaji wa magari (car wash,garage), viwanda, ufyatuaji wa tofali n.k.

 Kupitisha kwa Afisa Afya wa Manispaa kwa ajili ya usalama/usafi wa jengo kwa

ujumla. Kwa biashara za Hotel za kawaida, vilabu vya pombe,utengenezaji wa

vyakula.

(E) WAOMBAJI WA ZAMANI:

 

Waombaji wanaoendeleza/kuhuisha (Renewals)watapeleka maombi yao Ofisi ya

Biashara

Wakionyesha Nakala ya Leseni halisi iliyoisha muda wake.

 Wafanyabiashara hao baada ya kukamilisha taratibu za awali watatakiwa kwenda

Ofisi ya Mapato (TRA) kwa ajili ya kupatiwa Tax Clearance Certtificate.

 Mfanyabiashara baada ya kupatiwa Tax Clearance atarudi Ofisi ya Biashara kwa ajili

ya malipo ya Ada ya Leseni ambayo hulipiwa Benki (NMB).

 Baada ya malipo kufanyika Mfanyabiashara atarudi tena Ofisi ya Biashara kwa ajili

ya Leseni.

 Kwa sasa Leseni zinatolewa baada ya kuingiza taarifa za Mfanyabiashara kwenye

kompyuta.

 Baada ya zoezi la uingizaji taarifa za Mfanyabishara kukamilika mfanyabiashara

ataandikiwa Leseni.

 Ni vyema kuwahi kulipia kwani siku za kulipia Leseni bila faini ni siku 21tu.

(F) MAKOSA YA LESENI (SHERIA NA. 25 KIFUNGU 17 A-H)

1. Ukiendesha biashara bila Leseni ukibainika umetenda kosa (kifungu 17(A).)

2. Ukiendesha biashara sehemu ambayo haikutajwa kwenye Leseni ukibainika utakuwa

umetenda kosa (kifungu 17(I)(C).

 

3. Ukishindwa kuiweka Leseni ya biashara mahali pa wazi (Conspicuous Place) kwenye

biashara wakati wote wa biashara utakuwa umetenda kosa.

4. Ukishindwa kuonyesha Leseni unapotakiwa kuionyesha Leseni yako mara itakapohitajika

na mamlaka husika utakuwa umetenda kosa.

5. Kutoa taarifa za uongo wakati wa kuomba Leseni ni kosa.

6. Ukishindwa kuitoa au kuiwakilisha kwa Afisa mhusika Leseni ya biashara kwa wakati

unaotakiwa ni kosa Na. 15.

7. Kusema uongo kwa lengo la kupitishiwa ada isiyo kuwa sahihi ni kosa.

(G) MASHARTI YA KUTUMIA LESENI

 Kwamba hutaweka masharti yeyote kwa mnunuzi.

 Kwamba utatoa risiti kwa mauzo yoyote.

 Kwamba utafuata Sheria ya Leseni ya biashara ya 1972.

 Kwamba hutauza huduma ya bidhaa ambazo hazizingatii viwango vya ubora

vilivyowekwa na vyombo vinavyohusika kisheria.

 Kwamba Leseni hii inaweza kunyang’anywa wakati wowote ikiwa itaonekana kwamba

uliipata kwa udanganyifu au umekiuka masharti ya Leseni hii.

KUNDI LA PILI

SHERIA HII INAHUSU UUZAJI WA VILEO VYA KIGENI/KIENYEJI

(Sheria Na. 28 ya Mwaka 1968)

WAOMBAJI WAPYA MAOMBI YAO YAPITISHWE MAENEO YAFUATAYO:

 Kata

 Ardhi/Mipango Miji

 Afya

 Polisi

Bodi ya Vileo ya eneo husika ndio mamlaka ya ngazi ya mwisho ya Manispaa ya kuruhusu ni

nani apewe leseni na aruhusiwe kuuza aina gani ya vileo na muda wa kufanya biashara

Baada ya kulipia ada ya maombi ambayo kwa mujibu wa Sheria ni Ths. 2,000/= kwa kila ombi

 

KALENDA:

Leseni ya vileo huwa ni ya miezi sita yaani kuanzia tarehe 1 April hadi tarehe 30 Septemba kwa

Mwaka husika na kuanzia tarehe 1 Oktoba hadi 30 Machi mwaka unaofuata.

Baada ya kikao cha mwanzo Mamlaka inaweza kujadili na kutolea uamuzi maombi ambayo

hayakupitia kwenye kikao cha mwanzo kwa kulipia ada ya Shs. 8,000/= juu ya ada ya kawaida

ya maombi ambayo ni sh. 2,000/= na hivyo kufanya ada ya maombi kwa wanaoleta maombi nje

ya muda uliopangwa kuwa Tshs. 10,000/=

 

WAOMBAJI WA ZAMANI:

 Waombaji wanaondeleza/kuhuisha watapeleka maombi yao Ofisi ya Biashara

wakionyesha Nakala ya Leseni halisi iliyoisha muda wake.

 Wafanyabiashara hao baada ya kukamilisha taratibu za awali watatakiwa kwenda Ofisi

ya Mapato (TRA) kwa ajili ya kupatiwa Tax Clearance Certificate.

 Mfanyabiashara baada ya kupatiwa Tax Clearance atarudi Ofisi ya Biashara kwa ajili

ya malipo ya Ada ya Leseni ambayo hulipiwa Benki(NMB).

 Baada ya malipo kufanyika Mfanyabiashara atarudi tena Ofisi ya Biashara kwa ajili ya

Leseni.

 Kwa sasa Leseni zinatolewa baada ya kuingiza taarifa za Mfanyabiashara kwenye

kompyuta.

 Baada ya zoezi la uingizaji taarifa za Mfanyabishara kukamilika mfanyabiashara

ataandikiwa Leseni.

 Ni vyema kuwahi kulipia kwani siku za kulipia Ada ya Leseni bila faini ni siku 14 tu.

 

AINA YA LESENI:

1. Retailers on Licence – Bar

2. Retailers off Licence - Grocery – Off – Licence

3. Wholesale dealers Licence – Kuuza pombe za kigeni jumla

4. Member Club Licence – Leseni ya klabu ya wanachama

5. Local Liquor Licence – Leseni ya pombe za kienyeji

ADA YA LESENI YA VILEO:

Biashara za Vileo hazikufanyiwa marekebisho yeyote ya ada ya Leseni.

Leseni hizo zitaendelea kulipiwa ada ya Leseni kila baada ya miezi sita kama ifuatavyo:

 BAR - TSHS. 40,000.00

 GROCERY - TSHS. 30,000.00

 CLUBS - TSHS. 20,000.00

 WHOLESALE - TSHS. 20,000.00

 POMBE ZA KIENYEJI - TSHS. 12,000.00

 

MAKOSA CHINI YA SHERIA HII:

1. Kuendesha shughuli kabla au baada ya saa zilizoruhusiwa.

2. Kuhudumia wateja ambao ni chini ya umri ulioruhusiwa kisheria (miaka 18)

3. Kutokuiweka Leseni ya Vileo katika eneo husika wakati biashara inafanyika (Serving

point ) kwa mfano: Counter

4. Kuendesha vituo vya kuuzua (Serving points)zaidi ya kimoja kwa Leseni moja kwa

mujibu wa Sheria kila counter inatakiwa kuwa na Leseni yake.

 

SAA ZINAZOKUBADILIKA KISHERIA KWA WAFANYABIASHARA WA VILEO

KWA KUZINGATIA AINA YA LESENI ILIYOTOLEWA.

1. BAR (RETAILERS ON LICENCE):

(i) Jumatatu hadi Ijumaa:

(a) Saa 6:00 Mchana hadiSsaa 8:00 Mchana.

(b) Saa 12:00 hadi 5:00 Usiku.

(ii) Jumamosi, Jumapili na Siku za Sikukuu:

(a) Saa 5:00 Asubuhi hadi Saa 8:00 Mchana.

(b) Saa 11:00 Jioni hadi Saa 6:00 Usiku.

 

2. GROCERY AND WHOLESALE (RETAILERS OFF LICENCE &

WHOLESALE):

(i) Jumatatu hadi Ijumaa

(a) Saa 2:00 Asubuhi hadi Saa 1:00 Usiku

(ii) Jumamosi,Jumapili na Siku za Sikukuu:

(a) Saa 3:00 Asubuhi hadi Saa 6:00 Mchana

 

3. RESTAURANTS AND HOTELS:

(i) Jumatatu hadi Ijumaa

(a) Saa 6:00 Asubuhi hadi Saa 8:00 Mchana

(b) Saa 12:00 Jioni hadi Saa 5:00 Usiku

(ii) Jumamosi,Jumapili na siku za sikukuu:

(a) Saa 5:00 Asubuhi hadi Saa 8:00 Mchana.

(b) Saa 11:00 Jioni hadi Saa 6:00 Usiku.

 

4. MEMBERS CLUB (KLABU YA WANACHAMA):

Masharti yake kama Bar ila pombe ni mali ya Club na inanywewa na wanachama tu.

(i) Jumatatu hadi Ijumaa

(a) Saa 6:00 Mchana hadi Saa 8:00 Mchana

(b) Saa 12:00 Jioni hadi Saa 5:00 Usiku

(ii) Jumamosi,Jumapili na siku za Sikukuu

(a) Saa 5:00 Asubuhi hadi Saa 8:00 Mchana

(b) Saa 11:00 Jioni hadi Saa 6:00 Usiku

 

5. POMBE ZA KIENYEJI:

(i) Jumatatu hadi Ijumaa

(a) Saa 6:00 Mchana hadi Saa 8:00 Mchana

(b) Saa 12:00 Jioni hadi Saa 5:00 Usiku

(ii) Jumamosi,Jumapili na Siku za Sikukuu

(a) Saa 5:00 Asubuhi hadi Saa 8:00 Mchana

(b) Saa 11:00 Jioni hadi Saa 6:00 Usiku

 

UHAMISHO WA LESENI:

Kila Mfanyabiashara atakaye hamisha biashara kutoka eneo moja kwenda eneo jingine

anapaswa kuandika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kwa kupitia kwa Afisa Mtendaji wa

kata Biashara inakohamia na gharama za Uhamisho ni Shs Elfu kumi tu 10,000/=

 

UPOTEVU WA LESENI:

Mfanyabiashara aliyepoteza /kuibiwa Leseni anapaswa kutoa taarifa kituo cha polisi Wilaya ili

apewe kibali cha Upotevu wa Leseni (Loss report). Baada ya kupata kibali cha Upotevu

akipeleke katika Ofisi ya Halmashauri Kitengo cha Biashara na atalipishwa Tshs

20,000/=kwa ajili ya kupata Nakala ya Leseni.

 

KUFUNGA BIASHARA:

Kila Mfanyabiashara atakayesimamisha/kuacha kufanya biashara atapaswa kuandika barua kwa

Mkurugenzi wa Manispaa kupitia kwa Afisa Mtendaji wa Kata husika.

NB:

Pamoja na taratibu zilizoanishwa hapo juu Mfanyabiasha anapaswa kulipia Ada zifuatazo:

1. Ushuru wa Huduma (Service Levy)

2. Ada ya Mabango (Billboard Fee)

3. Hotel Levy kwa Biashara za Hotels,Guest house na Lodge (Hulipwa kila Mwezi)

4. Ada ya Ukaguzi wa Jengo la Biashara (Inspection Fee for Business premise)

5. Ada ya Uzoaji taka(Refuse Collection Fee)

6. Ada ya Upimaji Afya kwa wahudumu wa nyumba za kulala wageni na wauzaji

vyakula.(Medical Examination F

Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI SHULE YA SEKONDARI MAWENZI July 27, 2022
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI July 13, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MUDA YA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU September 21, 2020
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA(JOINING INSTRUCTIONS)KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI MANISPAA YA MOSHI 2021 December 18, 2020
  • Tazama

Habari Mpya

  • WANANCHI WA KATA YA MSARANGA WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUWAJENGEA SHULE YA SEKONDARI

    February 22, 2023
  • ZAIDI YA BILIONI 50.1 KUTUMIKA MANISPAA YA MOSHI 2023/2024

    February 14, 2023
  • MKUU WA WILAYA AWAPONGEZA WALIMU WA MANISPAA YA MOSHI

    January 10, 2023
  • MKUU WA WILAYA YA MOSHI AUPONGEZA UONGOZI WA MANISPAA KWA KUTOA MIKOPO YA SHS. 367,550,000.

    November 10, 2022
  • Tazama

video

LISHE KUWA AJENDA YA KUDUMU MANISPAA YA MOSHI
videos

Kurasa za Karibu

  • Instagram account

Tovuti Mashuhuri

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    MOSHI MANISPAA KILIMANJARO

    Sanduku la barua: P.O BOX 318 MOSHI

    Simu: +255-027-2752906

    simu ya Mkononi: +255-027-274371/4

    Barua Pepe: md@moshimc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Manispaa ya Moshi